
MASHARIKI YA ATLANTIKI YATINGISHWA: Biashara kati ya EU na Marekani katika Hatari Kubwa Kufutika kutokana na Tarifa Mpya ya Trump
BRUSSELS | LondonCNN — Umoja wa Ulaya (EU) umetangaza onyo kali dhidi ya mipango ya Marekani kuweka ushuru wa asilimia 30 kwa bidhaa zote zinazoingia kutoka barani Ulaya, hatua ambayo inaweza kuua kabisa biashara baina ya pande hizo mbili.
Kamishna wa Biashara wa EU, Maroš Šefčovič, alisema Jumatatu mjini Brussels kuwa endapo Rais Donald Trump ataendeleza azma yake ya kuanza kutekeleza ushuru huo kuanzia Agosti 1, biashara ya pande hizo mbili “itakuwa haiwezekani kabisa.”
“Tarifa ya asilimia 30 au zaidi ina athari sawa – kimsingi inakata kabisa biashara,” alisema Šefčovič kabla ya kikao cha mawaziri wa mambo ya nje wa EU.
Kwa mujibu wa Baraza la Ulaya, biashara ya bidhaa na huduma kati ya EU na Marekani ilifikia €1.68 trilioni ($1.96 trilioni) mwaka jana, ikiwa ni takriban asilimia 30 ya biashara ya kimataifa ya bidhaa na huduma. Hii ni moja ya uhusiano mkubwa zaidi wa kiuchumi duniani.
Lakini tangu kurejea madarakani mwezi Januari, Trump ameongeza – na kuahidi kuongeza zaidi – ushuru kwa mataifa mbalimbali kwa kile anachodai ni kulinda viwanda vya Marekani na kupunguza nakisi ya biashara.
Katika barua yake kwa EU siku ya Jumamosi, Trump alisisitiza kuwa ushuru huo wa asilimia 30 ni hatua ya “ushuru wa kulipiza kisasi” dhidi ya kile anachokiita vizingiti visivyo vya ushuru kama ushuru wa huduma za kidijitali na tarifa za EU dhidi ya bidhaa za Marekani.
🎯 EU: Tuko Tayari kwa Vita ya Biashara
Licha ya mvutano, EU imesisitiza kuwa bado ina matumaini ya kufikia makubaliano ya maelewano. Šefčovič alisema kuwa walikuwa “karibu sana” kufikia makubaliano kabla ya Trump kurusha tishio jipya.
Kwa hatua ya kujizuia, EU imechelewesha utekelezaji wa hatua za kulipiza kisasi dhidi ya bidhaa za Marekani zenye thamani ya €21 bilioni ($25 bilioni) hadi mapema mwezi Agosti – ikiwa ni nafasi ya mwisho kwa mazungumzo ya kidiplomasia.
Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Denmark, Lars Løkke Rasmussen, alisema waziwazi kuwa EU inapaswa kujiandaa kwa vita ya kiuchumi.
“Ukihitaji amani, lazima ujitayarishe kwa vita… hatuwezi kuendelea kuwa wavumilivu bila mipaka,” alisema Rasmussen kabla ya mkutano wa mawaziri.
📉 Athari Zakwishaanza Kuonekana
Masoko ya Ulaya tayari yameanza kuhisi mtikisiko wa tishio hilo. Stoxx Europe 600, kipimo kikuu cha masoko ya hisa barani Ulaya, kilishuka kwa asilimia 0.27 kufikia mchana wa Jumatatu saa za CET.
Katika mazingira haya ya mvutano wa kibiashara na kutokuwa na uhakika, mustakabali wa uhusiano wa kiuchumi kati ya mabara haya mawili unaonekana kuyumba, huku athari zikitishia kusambaa kutoka viwandani hadi mifuko ya walaji wa kawaida.
✍🏽 Imeandikwa na: MANGWA
